Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, February 11, 2017

UJERUMANI LEO YAFANYA UCHAGUZI WA RAIS

Ujerumani leo yafanya uchaguzi wa Rais

Baraza maalum la wajumbe na wawakilishi kutoka majimbo yote ya Ujerumani litakutana leo kumchagua rais mpya wa Ujerumani. Aliyekuwa waziri wa mambo ya nje Frank-Walter Steinmeier ndiye mwenye nafasi kubwa ya kuchaguliwa.
Bundesversammlung 2012 (picture-alliance/dpa/H. Hanschke)
Akiwa mwanasiasa anaependwa zaidi na umma hapa nchini Ujerumani Frank-Walter Steinmier atachukua wadhifa wa urais kutoka kwa Joachim Gauck mwenye umri wa miaka 76, mhubiri wa zamani na mwanaharakati wa kutetea demokrasia ambaye mwaka jana alisema hatawania muhula mwingine madarakani wa miaka mitano kwasababu ya umri wake.
Rais anachaguliwa na kongamano maalum la wajumbe 1260 bungeni mjini Berlin ambalo linajumuisha wabunge 630 na idadi kama hiyo ya wawakilishi wa majimbo yote 16 ya Ujerumani. Steinmeier anaungwa mkono na serikali baada ya Merkel kushindwa kumpata mgombea wa kihafidhina anayestahili kuwa rais.
Umaarufu wa chama cha SPD waongezeka
Licha ya kuwa kwa muda mrefu amekuwa mwanasiasa anayependwa Ujerumani, alishindwa kumuondoa madarakani Merkel katika uchaguzi wa Ukansela wa mwaka 2009. Uchaguzi wa leo unakuja wakati Ujerumani ikijiandaa kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Septemba mwaka huu ambapo Merkel anagombea muhula wa nne madarakani.
Wasocial Democrats hivi sasa wana uungwaji mkono mubwa kulingana na kura za maoni tangu kumteua aliyekuwa Rais wa bunge la Umoja wa Ulaya Martin Schulz kuwa mgombea wao wa Ukansela.
Frankreich Angela Merkel und Martin Schulz in Verdun (Getty Images/S. Gallup) Kansela Angela Merkel na mgombea Ukansela Martin Schulz
Kuimarika kwa chama cha SPD kunaongeza shinikizo kwa Merkel na chama chake kujiandaa vyema na kufanya kampeini kali kuelekea uchaguzi. Lakini kuchaguliwa kwa Rais ambaye miongoni mwa majukumu yake ni kuteua serikali mpya na majaji kumeonyesha kuwa kibarua kigumu kwa Merkel.
Tofauti na Gauck ambaye hakuwa anaegemea chama chochote cha kisiasa, Steinmeier amekuwa katika siasa za Ujerumani kwa muda mrefu. Kama mnadhimu mkuu wa Kansela Gehard Schroeder alikuwa miongoni mwa waasisi wakuu wa mageuzi ya kiuchumi mwaka 2003, mageuzi yanayotajwa kuchangia Ujerumani kuwa nchi imara kiuchumi.
Steinmeier ndiye mwanasiasa anayependwa zaidi Ujerumani
Chini ya utawala wa Merkel, amehudumu mara mbili kama waziri wa mambo ya nje kuanzia mwaka 2005 hadi 2009 na tena kuanzia mwaka 2013 hadi mwaka huu. Anaheshimika pakubwa kwa kujaribu kuutatua mzozo wa Ukraine. Mwanasiasa huyo ambaye ni mwanadiplomasia mtajika, alimshutumu vikali Donald Trump wakati wa kampeini za uchaguzi wa rais wa Marekani.
Deutschland Joachim Gauck und Frank-Walter Steinmeier (picture-alliance/dpa/B. Pedersen) Rais wa Ujerumani Joachim Gauck na mgombea urais Frank Walter Steinmeier
Alipoulizwa mwezi Agosti kuhusu kuongezeka kwa siasa kali za kizalendo Ujerumani na kwingineko, Steinmeier aliwashutumu wale aliowataja wanaofanya siasa za kuingiza uoga, akikitaja chama cha mrengo wa kulia cha siasa kali zinazowapinga wahamiaji Ujerumani Alternative für Deutschland AfD, waliopelekea Uingereza kujiondoa kutoka Umoja wa Ulaya na wanaoeneza chuki kama Donald Trump.
Alipoteuliwa kugombea urais mwezi Novemba, Steinmeier alitoa wito wa kuwepo imani wakati ulimwngu unapokumbwa na mizozo akiongeza Rais wa Ujerumani sharti awe mtu ambaye harahisishi mambo bali anayewatia moyo watu. Merkel amemsifu Steinmeier na kumtaja kuwa ni kiongozi wa maana na mwafaka wakati ambapo kuna msukosuko na hali ya sintofahamu ulimwenguni.
Steinmeier anakabiliwa na upinzani kutoka kwa wagombea wengine watatu akiwemo Alexander Hold wa chama kidogo cha siasa za wastani za mrengo  wa kulia- Freie Waehler, mtafiti kuhusu umasikini Christoph Butterwegge wa chama cha mrengo wa kushoto cha Die Linke na Albrecht Glaser wa chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha Alternative for Deutschland AfD

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages