Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, February 18, 2017

MAGAIDI WAWILI WAANGAMIZWA MAGHARIBI MWA TUNISIA

Wizara ya Ulinzi ya Tunisia imetangaza kuwa, magaidi wawili wakufurishaji wameangamizwa katika maeneo ya milimani ya jimbo la Kasserine la magharibi mwa nchi hiyo katika operesheni maalumu ya jeshi ya kupambana na magenge ya kigaidi.
Televisheni ya Sky News imeinukuu Wizara ya Ulinzi ya Tunisia ikitangaza habari hiyo jana na kuongeza kuwa, jeshi la nchi hiyo limepambana na magaidi katika milima ya al Samamah ya jimbo la Kasserine, karibu na mpaka wa nchi hiyo na Algeria na kufanikiwa kuangamiza magaidi wawili na kuwatia mbaroni magaidi wengine kadhaa.
Taarifa ya Wizara ya Ulinzi ya Tunisia imetangaza pia habari ya kutekwa idadi kubwa ya silaha kutoka kwa magaidi hao, kwenye operesheni hiyo.
Eneo hilo la mpakani mwa Tunisia na Algeria linatumiwa sana na magaidi wakufurishaji kufanya mashambulizi ndani ya nchi hizo mbili.
Wakati huo huo, viongozi wa serikali ya Tunisia, siku ya Alkhamisi waliongeza muda wa hali ya hatari nchini humo kwa miezi mitatu zaidi kuanzisha tarehe 16 Februari.
Askari wa Tunisia katika opereseheni ya kupambana na magaidi

Magenge ya kigaidi yameongeza harakati zao nchini Tunisia tangu mwaka 2011 baada ya kutokea mapinduzi ya wananchi yaliyoungóa madarakani utawala wa dikteta Ben Ali.
Hadi hivi sasa makumi ya watu wameshauawa wakiwemo wanajeshi, polisi, raia wa kawaida na watalii.
Viongozi wa Tunisia wameimarisha ulinzi katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo tangu mwaka 2015 baada ya kuuawa askari 12 wa gadi ya Rais na pia shambulio la kikatili lililotokea mwaka 2016 karibu na mpaka wa nchi hiyo na Libya.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages