Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, February 25, 2017

UHUSIANO KATI YA TRUMP NA WANAHABARI WAZIDI KUZOROTA

Rais wa Marekani Donald Trump amesema hatahudhuria dhifa ya chakula cha jioni inayoandaliwa na chama cha waandishi wa habari wanaoripoti matukio ya Ikulu.
Washington Donald Trump beim traditionellen Korrespondenten-Galadinner im Weißen Haus (Getty Images/L. Busacca)
Tangazo la Trump linakuja siku moja baada ya kuwashutumu vikali wanahabari kwa kuwataja kuwa ni adui wa watu kwa kudai wanaeneza taarifa za uongo na za kupotosha. Kiongozi huyo mpya wa Marekani pia amewataja wanahabari kuwa chama cha upinzani nchini Marekani. Dhifa hiyo iliyoanzishwa mwaka 1921, huwa inahudhuriwa na watu mashuhuri, wanasiasa wa Marekani na wanahabari.
Rais wa chama cha waandishi wa habari wa Ikulu ya White House WHCA Jeff Mason amesema dhifa hiyo itaendelea kama ilivyopangwa kwani ni desturi ya kusherehekea mchango muhimu unaotekelezwa na mashirika ya habari katika taifa lililo huru, kusherehekea uhuru, kuangazia mafanikio ya uandishi habari katika ulingo wa kisiasa na kuwatambua wanafunzi bora wanaosomea uandishi ambao wanawakilisha kizazi kijacho cha tasnia hiyo ya habari.
Washington Barack Obama beim traditionellen Korrespondenten-Galadinner im Weißen Haus (Getty Images/O. Douliery-Pool) Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama katika dhifa ya 2016
Trump awataja wanahabari wapinzani
Msemaji wa Ikulu Sean Spicer mnamo siku ya Ijumaa aliwazuia wanahabari wa mashirika kadhaa kuhudhuria kikao cha wanahabari katika Ikulu. Wanahabari wa Mashirikia ya CNN, New York Times, Politico, Los Angeles Times na Buzzfeed hawakuruhusiwa kuhudhuria kikao cha wanahabari katika ofisi ya msemaji wa Ikulu ya Rais wa Marekani.
Katika kipindi cha kampeini mwaka jana, kundi la Trump liliyapiga marufuku mashirika kadhaa likiwemo gazeti la Washington Post na Buzzfeed dhidi ya kuripoti katika mikutano ya kampeini likiyashutumu kwa upotoshaji ba kueneza habari za uongo.
Spicer amesema Ikulu ya Marekani inapanga kupambana dhidi ya kile alichokitaja kuangaziwa kionevu na vyombo vya habari. Msemaji huyo wa Ikulu ameeleza kuwa hawatakaa tu na kuruhusu taaarifa za uongo na za kupotosha zikitolewa.
Uhuru au upotoshaji wa habari?
Hatua hiyo ya utawala wa Trump kuyashambulia mashirika ya habari nchini Marekani imeashutumiwa vikali na makundi ya wanahabari na vyomvo hivyo vya habari.
Taarifa kutoka kwa mhariri mkuu wa The New York Times Dean Baquet ilisema jambo kama hilo halijawahi kutokea katika Ikulu ya Rais ya White House katika historia yao ndefu ya kuripoti taarifa kutoka tawala chungu nzima kutoka vyama tofauti vya kisiasa nchini Marekani.
USA Weißes Haus - Sean Spicer (picture-alliance/newscom/UPI Photo/P. Benic) Msemaji wa Ikulu ya Rais Sean Spicer
Baquet alisema wanapinga vikali kuzuiwa kwa gazeti lao na mashirika mengine ya habari na kuongeza kuruhusiwa kwa vyombo hivyo kuwa na uhuru na kuangazia matukio ya serikali iliyo wazi bila shaka ni muhimu kwa maslahi ya taifa.
Wakati wa kampeini zake kuingia madarakani, Trump mwenye umri wa miaka 70 aliyashutumu vikali mashirika makuu ya habari ya Marekani kwa kuwa na upendeleo na amezidisha shutuma hizo baada ya kuingia madarkani kwa kudai wanahabari wanaangazia zaidi mapungufu yake badala ya kuangazia mafanikio yake.
Stephen Bannon, mkuu wa mipango na mshauri mwandamizi wa Trump ambaye pia ni mkuu wa tovuti ya kihafidhina ya Breitbart, amebadhiri kuwa uhusiano kati ya utawala huo mpya wa Marekani na wanahabari ambao amewataja wapinzani utazidi tu kuwa mbaya jinsi rais huyo wa Marekani anavyozidi kutoa ajenda zake.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages