Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, February 22, 2017

BARAZA LA MAWAZIRILAUNGA MKONO HATUA ZA KUREJESHWA MAKWAO HARAKA WAHAMIAJI

Baraza la mawaziri la serikali kuu ya Ujerumani limeunga mkono makubaliano yaliyofikiwa kati ya serikali kuu na zile za majimbo ya kurejeshwa makwao haraka wahamiaji wasiokuwa na nafasi ya kukubaliwa kinga ya ukimbizi. Habari hizo zimetangazwa na waziri wa mambo ya ndani Thomas de Maizière mwishoni mwa kikao hicho cha baraza la mawaziri. Mswaada huo wa sheria unalitaka shirika linalosimamia masuala ya wahamiaji na wakimbizi lisikilize simu za mkononi za wahamiaji ikilazimika ili kupata maelezo ya vitambulisho vyao. Zaidi ya hayo muda wa kushikilwa wahamiaji utarefushwa wakionekana wanaweza kuhatarisha usalama wa nchi. Kwa mujibu wa waziri de Maizière, baraza la mawaziri limeunga mkono fikra ya kufungwa kikuku cha elektroniki mguuni,yeyote yule atakaekwepa kushirikiana na maafisa wa uhamiaji.Makubaliano hayo yalifikiwa february tisa iliyopita kati ya kansela Merkel na mawaziri wakuu wa serikali za majimbo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages