Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, February 19, 2017

UGANDA YAKAMATA TANI MOJA YA MENO YA TEMBO

Serikali ya Uganda imefanikiwa kuiweka kizuizini tani moja ya pembe za ndovu na kuwakamata raia watatu wa mataifa ya Afrika Magharibu kwa tuhuma za kupanga njama za kutaka kuisafirisha mataifa ya nje. Msemaji wa mamlaka ya wanyamapori Gessa Simplicious amesema shehena hiyo ilikamatwa Ijumaa jioni katika nyumba moja ya kifahari iliyoko katika viunga vya jiji la Kampala. Raia wa Liberia na wenzake wawili wa Guinea-Bissau wametiwa mbaroni na kwamba watafikishwa mahakamani kwa madai ya uhalifu. Afisa huyo wa mamlaka ya wanyamapori amesema pembe hizo za ndovu zinaonekana kama zimeingizwa nchini humo kutokea matifa jirani na Uganda kama vile Tanzania na Congo kwa kuwa alama zake hazifanani na za Uganda. Afrika ambayo ilikuwa na jumla ya tembo milioni 1.3 miaka ya sabini kwa hivi sasa imesalia na laki tano tu, kutokana na vitendo vya ujangili.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages