Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, February 10, 2017

22 BAHMAN, SIKU YA KUDHIHIRISHA UWEZO NA MSHIKAMANO WA TAIFA LA IRAN

Hii leo Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran yametimiza miaka 38 tangu yalipopata ushindi mwaka 1979. Tukio hilo muhimu katika historia ya Iran na dunia nzima bado linapewa umuhimu mkubwa na wanafikra na waandishi na limekuwa kigezo na ruwaza njema kwa wapigania uhuru, haki na uadilifu kote duniani.
Ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ulivuruga kabisa mahesabu ya mabeberu na kutoa ilhamu ya darsa la kusimama kidete na kupambana na dhulma na madola ya kidhalimu.  
Rais Rouhani akihutubia mamilioni ya wananchi, Medani ya Azadi mjini Tehran
Mapambano ya wananchi wa Iran yalianza pale taifa lilipochukua uamuzi wa kuwa huru na kujitawala kwa ajili ya maendeleo na ufanisi, suala ambalo lilikwenda kinyume na maslahi na matakwa ya madola ya kibeberu. Fikra ya harakati hiyo ya kimapinduzi ilivuka mipaka ya Iran na kuwa kigezo bora cha kusimama kidete na chachu ya kukabiliana na madola makubwa. Kwa sababu hiyo maadui wamezidisha njama za kutaka kuyabinya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na kuzuia ujumbe wake wa kimataifa kwa kutumia njia mbalimbali. Ni wazi kuwa, mpambano huo utaendelea kuwepo maadamu taifa la Iran linaendelea kusimama kidete kwa ajili ya kukabiliana na sera za kutaka makuu na kujipanua zaidi. Pamoja na hayo kuna matatizo na vizingiti vingi katika njia hiyo ya mapambano dhidi ya mabeberu kuanzia kwenye masuala ya kiuchumi hadi kwenye vitisho vya mashambulizi ya kijeshi. Mapambano katika uwanja huu ni magumu sana na yanahitaji azma kubwa, imani ya kweli na misimamo madhubuti. Vilevile sharti la kufanikiwa katika mapambano hayo ni umoja na mshikamano.
Maandamano ya mamilio ya Wairani mjini Tehran 10/02/17
Kwa miaka mingi sasa maadui wa taifa la Iran wameanzisha mashambulizi makali ya kipropaganda na ya vyombo vya habari dhidi ya utawala wa Kiislamu wa Iran tena kwa kutumia gharama kubwa ya fedha kwa lengo ya kuficha mafanikio ya Iran ya Kiislamu na kudhihirisha baadhi ya nukta hasi ili kuwakatisha tamaa na matumaini wananchi hususan tabaka la vijana. Uadui huo unalenga msingi na utambulisho wa utawala wa Kiislamu. Uhasama na uadui huo daima umekuwa ukionekana katika matamshi na vitendo vya viongozi wa serikali ya Marekani. Kama alivyosema Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran, Ayatullah Ali Khamenei kwamba, mwenendo huo unaonesha kuwa, dhati ya Marekani haibadiliki, na kwamba hakuna tofauti yoyote baina ya serikali za Wademocrat na zile za Warepublican katika kulifanyia uadui taifa la Iran na Waislamu kwa ujumla. 
Donald Trump na Barack Obama
Wachambuzi na wanadharia wengi mashuhuri duniani wanakubaliana kwamba, licha ya kupita karibu miongo minne sasa ya uhai wake, Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran hayajatengana na kuachana na malengo na thamani zake za awali licha ya vizingiti, mikingamo na uhasama wa Marekani na mabeberu wenzake na kwamba, taifa la Iran lingali linasonga mbele katika safu moja na yenye mshikamano. Kwa mshikamano na umoja huo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeweza kuthabitisha nafasi yake katika eneo la Mashariki ya Kati na duniani licha ya kuwepo mashinikizo na njama nyingi kuanzia vita vya kulazimishwa, mzingiro wa kiuchumi na vikwazo vya pande zote vya kidhalimu. Hii ina maana kwamba, kusimama kidete kwa taifa la Iran mbele ya madola ya kibeberu si nara na maneno matupu. 
Maadhimisho ya ushindi wa Mapindzi ya Kiislamu nchini Iran
Watu wanaoelewa vyema fikra za Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran wanajua kuwa mahudhurio na kushiriki kwa mamilioni ya wananchi katika maandamano ya leo ya kuadhimisha ushindi wa mapinduzi hayo ni tangazo za kushikamana wananchi na malengo, fikra na sera za Mapinduzi ya Kiislamu na mwasisi wake hayati Imam Ruhullah Khomeini na ni dhihirisho la kuendelea kusimama kidete kwa taifa la Iran mbele ya uadui na njama za mabeberu wa dunia ya leo. Ujumbe wa maandamano ya mamilioni ya Wairan hii leo pia ni jibu kwa vitisho, bwabwaja na eti 'machaguo yaliyo juu ya meza' ya viongozi wa White House.  

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages