Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, February 17, 2017

LIGI YA MABINGWA YAINGIA HATUA YA MCHUJO

Ligi ya Mabingwa barani Ulaya inarejea huku kukiwa na mechi kadhaa za kusisimua hasa katika mechi za kwanza nne za mkondo kwa kwanza wa hatua ya 16 za mwisho
Champions League Arsenal vs Bayern (Reuters/D. Levepic)
Jumanne, Barcelona watakuwa mjini Paris kupambana na PSG ikiwa ni kwa mara ya tatu katika misimu minne katika hatua ya mwondowano. Barca walishinda katika robo fainali za 2013 na 2015 na wakashinda taji msimu huo. Pia utawaleta pamoja washambuliaji wa Uruguay, ambapo Edison Cavani wa PSG atakutana na Luis Suarez
Benfica na Borussia Dortmund, wote wakiwa mabingwa wa zamani, wanakutana katika mtanange ambao timu zote zinaonekana kuwa zenye uwezo sawa. Dortmund walikuwa wakali sana katika hatua ya makundi ambapo walimaliza katika nafasi ya kwanza mbele ya Real. Hata hivyo BVB hawajawa imara sana katika ligi ya nyumbani wakati Benfica wamepoteza mara mbili tu katika mechi zake 20 za nyumbani dhidi ya wapinzani wa Ujerumani.
Siku ya Jumatano, mjini Munich, Arsenal watajaribu kutafuta ushindi dhidi ya adui wanayemfahamu vizuri sana, Bayern. Timu hizo zinakutana kwa mara ya nne katika misimu mitano huku The Gunners wakitumai kuepuka kubanduliwa nje katika hatua hii kwa mwaka wa saba mfululizo. Viwili kati ya vichapo hivyo vilikuwa mikononi mwa Bayern mwaka wa 2013 na 2014
Real Madrid wana mtihani mkali dhidi ya Napoli, ambao hawajashindwa katika mechi 18, wakati wakilenga kuwa timu ya kwanza kuhifadhi kombe la Ligi ya Mabingwa. Aliyekuwa nyota wa Argentina Diego Maradona anatarajiwa kujiunga na mashabiki 10,000 wa Napoli watakaomiminika katika uwanja wa Santiago Bernabeu. Maradona alikuwa nahodha wa Napoli
Michuano minne ya mkondo wa kwanza itachezwa wiki ijayo, wakati ya marudiano ikichezwa Machi 7/8 na 14/15

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages