Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, February 19, 2017

RUSSIA: MAKOMBORA YETU YANA UWEZO WA KUPENYA KIRAHISI NGAO ZA MAREKANI

Naibu Waziri Mkuu wa Russia katika masuala ya ulinzi amesema kuwa, Moscow inatengeneza makombora ambayo yana uwezo wa kupenya kirahisi ngome za kujilinda na makombora za Marekani na kupiga kulikokusudiwa.
Shirika la habari la IRNA limemnukuu Dmitry Rogozin akisema hayo jana usiku na kuongeza kuwa, makombora ya Russia yana uwezo wa kukwepa ngao za kujilinda na makombora za Marekani zilizopo hivi sasa na zitakazokuja.
Amesema, ngao za kujilinda na makombora za Marekani hazina hatari yoyote hivi sasa kwa Russia zaidi ya kufanya uchokozi tu.
Dmitry Rogozin, Naibu Waziri Mkuu wa Russia katika masuala ya ulinzi

Itakumbukwa kuwa, tangu miaka mitatu iliyopita, Marekani ilianza kuweka ngao zake za kujilinda na makombora katika nchi za Ulaya Mashariki kwa madai ya kukabiliana na tishio la makombora ya Russia na imeweka miundombinu za ngao zake hizo katika nchi za Romania na  Poland.
Kitendo cha Marekani cha kuweka ngao zake za kujilinda kwa makombora huko Ulaya Mashariki kimewakasirisha viongozi wa Russia.
Moscow imetangaza kuwa, hatua hiyo ya Marekani ni tishio la wazi kwa usalama wa kiistratijia wa Russia.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages