Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, February 15, 2017

MAHAKAMA YA RUFAA KENYA YAWAACHILIA HURU VIONGOZI WA MADAKTARI

Mahakama ya Rufaa nchini Kenya leo imetoa amri ya kuachiliwa huru viongozi wa muungano wa madaktari na kusema kwamba, sasa wanaweza kufanya mazungumzo na serikali kuhusiana na mgomo katika sekta ya afya ambao umekwamisha pakubwa huduma katika sekta hiyo.
Katika taarifa yake, Mahakama ya Rufaa nchini Kenya imeamua viongozi wa chama cha wahudumu wa afya waliokuwa wamefungwa jela mwezi mmoja waachiliwe huru mara moja.
Viongozi saba wa madaktari nchini Kenya walifungwa Jumatatu baada ya kupatikana na hatia ya kutofuata uamuzi wa mahakama wa kumaliza mgomo wa madaktari ambao umedumu kwa miezi miwili na nusu sasa. Viongozi hao wametakiwa kuhakikisha suluhu ya mgomo huo inapatikana katika kipindi cha siku saba zijazo.
Mazungumzo ya kutafuta suluhu yataongozwa na Chama cha Wanasheria Kenya (LSK) na Tume ya Taifa ya Haki za Kibinadamu (KNHCR).
Mgomo wa madaktari Kenya
Madaktari wamekuwa wakiitaka serikali ya Kenya kuheshimu makubaliano ya mwaka 2013 ya kuwaongezea mishahara na kuboresha mazingira ya utendaji kazi hospitalini
Wanataka pia serikali iwekeze zaidi katika dawa, vifaa na mitambo hospitalini pamoja na kutoa pesa zaidi za kufadhili utafiti wa kimatibabu. Wamekataa mshahara walioongezewa na serikali wa asilimia 40 wakisema kuwa ni wa chini kuliko ule walioafikiana mwaka 2013. Karibu madaktari na wauguzi 5,000 kutoka hospitali 2,000 za umma nchini Kenya, walianza mgomo wiki ya kwanza ya mwezi Desemba na wagonjwa wamekuwa wakikosa matibabu. Mgomo huo wa madaktari umewakasirisha mno Wakenya na kuwa changamoto kubwa kwa serikali ya Rais Uhuru Kenyatta anayetarajiwa kutetea kiti chake katika uchaguzi ujao wa Agosti mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages