Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, February 20, 2017

PANCE AWAHAKIKISHIA VIONGOZI WA ULAYA MSAADA WA MAREKANI

Makamu wa rais wa Marekani Mike Pence amewakikishia viongozi wa Umoja wa Ulaya na NATO kwamba rais wa Marekani Donald Trump amejitolea kwa dhati kuyaendeleza mahusiano na mataifa ya Ulaya leo (20.02.2017) mjini Brussels.
EU - USA Mike Pence & Jean-Claude Juncker in Brüssel (Getty Images/AFP/E. Dunand) Makamu wa rais wa Marekani, Mike Pence (kulia) na Jean-Claude Juncker
Pence amekutana na viongozi wa Umoja wa Ulaya mjini Brussels, Ubelgiji, kituo chake cha mwisho cha ziara yake barani Ulaya, inayolenga kuwatuliza viongozi wa nchi washirika wa Ulaya kwamba rais Trump atawatelekeza. Akizungumza baada ya kukutana na rais wa Umoja wa Ulaya Donald Tusk, Pence amesema Marekani imejitolea kwa dhati kuundeleza ushirikiano na uhusiano na Umoja wa Ulaya.
Kiongozi huyo aidha amesema licha ya tofauti zilizopo, mabara ya Ulaya na Amerika yana utamaduni na maadili yanayofanana, na juu ya yote yana lengo moja la kuimarisha amani na maendeleo kupitia uhuru, demokrasia na utawala wa sheria, na Marekani itaendelea kujitolea daima kuyatimiza malengo hayo.
"Tunataka kuchukua hatua na tunautolea mwito Umoja wa Ulaya uungane na Marekani kuendelea kuimarisha juhudi za kukikabili kitisho cha ugaidi barani Ulaya. Ushirikiano zaidi utahitajika pamoja na kubadilishana taarifa za kijasusi kati ya nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya na kati ya Umoja wa Ulaya na NATO. Na Marekani itautanua ushirikiano huo kwa lengo la kuwalinda raia wetu."
Pence ameahidi Marekani itaendelea kushirikiana na Ulaya kuimarisha uchumi wa kanda hizo mbili kubwa duniani, kupambana na ugaidi na kuyalinda mataifa ya Ulaya Mashariki ambayo ni wanachama wa Umoja wa Ulaya dhidi ya Urusi.
Mengi yamebadilika Marekani na Ulaya
Tusk, ambaye ni waziri mkuu wa zamani wa Poland, kwa upande wake amesema mengi yametokea Marekani na Ulaya katika kipindi cha mwezi mmoja na ukweli uliopo ni kuwa mambo yamebadilika na hayako jinsi yalivyokuwa zamani. Amesema usalama wa Ulaya unaitegemea jumuiya ya kujihami ya NATO na ushirikiano wa karibu na Marekani kadri iwezekanavyo na kwamba Ulaya inategemea msaada wa Marekani.
EU - USA Mike Pence & Donald Tusk in Brüssel (picture-alliance/AP Photo/T. Monasse) Mike Pence, kushoto, akiwa na Donald Tusk
"Sharti tufanye kazi pamoja kuimarisha mifumo ya ushirikiano huu uwe wa kisasa, lakini pia tunatakiwa tukubaliane kuhusu jambo moja. Wazo kwamba jumuiya ya NATO haijapitwa na wakati, kama yalivyo maadili yaliyojikiti katika misingi yake. Tujadili kila kitu, tukianzia utoaji michango ya kifedha lakini kwa lengo la kuiimarisha NATO na wala sio kuidhoofisha," alisema Tusk.
Pence amekutana pia na rais wa kamisheni ya Umoja wa Ulaya, Jean-Claude Juncker, ambaye amesititiza kwamba Marekani inaihitaji Ulaya iliyoungana. Juncker, ambaye ni waziri mkuu wa zamani wa Luxembourg, pia amehimiza mshikamano katika Umoja wa Ulaya akisema huu sio wakati wa Ulaya kugawika katika mataifa na mikoa kama ilivyokuwa zamani.
Maandamano yafanyika
Waandamaji kadhaa walikusanyika nje ya makao makuu ya Umoja wa Ulaya mjini Brussels wakati wa zaira ya Pence, kuukosoa msimamo wa serikali ya rais Trump kuhusu wanawake, mashoga na mabadiliko ya tabai nchi. Usalama uliimarishwa maradufu katika eneo la majengo ya Umoja wa Ulaya wakati wa ziara ya kiongozi huyo.
USA Protest gegen Pence Besuch in Brüssel (DW/T. Schultz) Wanawake walioandamana wakiwa nusu uchi Brussels
"Tuko hapa kuandamana dhidi ya ziara ya Pence kwa sababu tumechukizwa na uamuzi wa utawala wa Marekani kuhujumu haki za wanawake ulimwenguni kote," alisema Irene Donadio, anayefanya kazi na shirika la kimataifa la uzazi wa mpango, wakati alipozungumza na shirika la habari la Ufaransa, AFP.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages