Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, February 17, 2017

MKUTANO WA USALAMA WAANZA MUNICH

Viongozi wa ngazi ya juu wa kidunia, wanadiplomasia na maafisa wa masuala ya ulinzi wanakutana kwa mara ya kwanza na maafisa wa utawala mpya wa Marekani chini ya Rais Donald Trump mjini Munich.
Deutschland Münchener Sicherheitskonferenz (Getty Images/AFP/T. Kienzle)
Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence, waziri wa ulinzi Jim Mattis na waziri wa nchi hiyo wa mambo ya ndani John Kelly wanaoongoza ujumbe wa Marekani katika mkutano unaohusu masuala ya ulinzi unaoanza leo mjini Munich, Ujerumani.
Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, Rais wa Baraza la Ulaya, Donald Tusk, na Katibu Mkuu wa NATO, Jens Stoltenberg, ni miongoni mwa viongozi wanaotarajiwa kushiriki mkutano huo ambao unatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi wa nchi zaidi ya 30 pamoja na mawaziri 80 wa wizara ya mambo ya nje na ulinzi pamoja na maafisa kadhaa.
Mkutano huo unafanyika mnamo wakati Rais Trump akiwa tayari ametoa kauli kadhaa kuhusiana na Jumuiya hiyo ya kujihami ya nchi za magharibi na hivi karibuni  akitoa kauli inayooonyesha kukubaliana na umuhimu wa ushirikiano huo wa kijeshi. Hata hivyo, amesisitiza juu ya  haja ya kila nchi mwanachama  wa ushirikiano huo kulipa gharama sawa zinazohusiana na masuala ya ulinzi jambo ambalo viongozi wa NATO wamekuwa wakilipigania kwa muda mrefu.

Marekani yaunga  mkono ushirikiano wa  NATO
US Wahl Mike Pence Vizepräsident in Newton (Reuter/S. Morgan) Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence
Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Jim Mattis, aliawaeleza mawaziri wa ulinzi wa nchi nyingine 27 zinazounda Jumuiya ya NATO  jumatano wiki hii mjini Brussels kuwa  Rais Trump anaunga mkono kwa kiwango cha juu NATO  na Katibu Mkuu wa NATO, Jens Stoltenberg, juu ya umuhimu wa ushirikiano huo wa NATO kwa Marekani.
Aidha waziri huyo wa ulinzi wa Marekani aliwaeleza washirika wenzake katika NATO kuwa wanapaswa kuongeza gharama za matumizi yao kijeshi kufikia mwishoni mwa mwaka huu vinginevyo huenda Marekani ikapunguza mchango wake kifedha katika NATO.
Masuala mengine ambayo yanaibua  maswali mengi ni  kuhusiana na hatua ya Rais Trump kuunga mkono hatua ya Uingereza kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya, ukaribu wake na Urusi na ahadi yake ya Marekanani kwanza.  Alisema muandaaji wa mkutano huo Wolfgang Ischinger ambaye ni balozi wa zamani wa Ujerumani nchini Marekani.
Ischinger amesema matarajio ya Makamu wa Rais wa Marekani, Mike Pence, kuzungumza hapo kesho katika mkutano huo ni makubwa sana.  Washiriki wa mkutano huo  wamesema wanatarajia kupata ufafanuzi kutoka kwa  makamu huyo wa Rais wa Marekani kuhusiana na msimamo wa Marekani juu ya uhusiano wake na Urusi, suala la NATO, Umoja wa Ulaya, biashara huru, masuala ya haki za binadamu na makubaliano ya nyukilia kuhusu Iran.
Masuala mengine ni pamoja na suala linalohusu ushirikiano kati ya Marekani na China na pia mgogoro wa Syria ambayo washiriki wa mkutano huo wanatarajia kupata majibu kuhusiana na maswali yaliyoibuka kuhusiana na msimamo wa Marekani katika masuala hayo.
Kansela Merkel ambaye anatofautiana kwa hoja na msimamo wa Rais Trump katika masuala hayo anatarajiwa pia kuhutubia mkutano huo hapo kesho.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages