Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, February 26, 2017

WATOTO 6 WAUAWA SHAHIDI KATIKA HUJUMA YA SAUDIA YEMEN

Watu wasipoungua 8 wakiwemo watoto sita wameuawa shahidi katika hujuma ya hivi karibuni ya ndege za kivita za Saudia katika maeneo mbali mbali nchini Yemen.
Kwa mujibu wa taarifa, siku ya Jumamosi ndege za kivita za Saudia zilishambulia mji wa bandarini wa Mukha katika Bandari ya Sham yapata kilomita 346 kusini mwa mji mkuu, Sana'a ambapo watoto watano wameuawa shahidi.
Aidha mke na mume na mtoto wao wamepoteza maisha baada ya ndege za kivita za Saudia kudondosha mabomu katika nyumba moja iliyo katika kijiji cha Manjada katika mkoa wa Dhamar, kusini magharibi mwa Yemen.
Hali kadhalka jana jioni ndege za kivita za Saudia zililenga kituo cha kijeshi cha Khalid katika Wilaya ya Mawza kaskazini magharibi mwa mkoa wa Ta'izz.
Katika kulipiza kisasi jinai hizo za Saudia, wapiganaji wa Kamati za Wananchi wamewapiga risasi na kuwaua wanajeshi wawili wa Saudi Arabia katika eneo la mkoa Jizan. 
Makao ya raia yaliyoharibiwa kwa mabaomu ya ndege za kivita za Saudi
Wakati huo huo Mkurugenzi wa Utalii Yemen Abdulrahman al-Na'mi amesema jeshi la Saudia limehujumu na kuharibu zaidi ya maeneo 200 ya kitalii nchini Yemen na kuisababishia nchi hiyo hasara ya dola bilioni 4.5 tokea Machi mwaka 2015 hadi sasa. Aidha amesema hujuma hiyo ya Saudia Yemen imepeleke karibu watu 90,000 kupoteza ajira katika sekta ya utalii.
Saudia, kwa kushirikiana na waitifaki wake, ilianzisha hujuma za kila upande dhidi ya Yemen tarehe 26 Machi mwaka 2015 kwa lengo la kumrejesha madarakani kibaraka wake Abdrabbuh Mansur Hadi rais wa zamani wa Yemen ambaye alijiuzulu nafasi hiyo na kukimbilia Saudia.
Hata hivyo licha ya Riyadh kufanya mauaji na uharibifu mkubwa nchini Yemen, imeshindwa kufikia malengo yake haramu nchini humo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages