Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, February 7, 2017

RWANDA YAWAFUTA KAZI MAKUMI YA POLISI KWA KULA RUSHWA

Serikali ya Rwanda imewafukuza kazi maafisa polisi 200 waliohusishwa na ufisadi nchini humo. Uchunguzi wa hivi karibuni uliofanywa na Taasisi ya Transparency International umeonyesha kuwa Rwanda ni nchi ya tatu yenye ufisadi wa kiwango cha chini katika nchi za chini ya Jangwa la Sahara barani Afrika.
Bi Marie- Imamaculate Ingabire Mkuu wa Taasisi ya Transparencyy International nchini Rwanda amesema kuwa kuorodheshwa Rwanda kuwa nchi yenye ufisadi wa kiwango cha chini kunadhihirisha azma iliyonayo serikali katika kukomesha ufisadi nchini humo. Serikali ya Rwanda iliidhinisha kufukuzwa maafisa hao wa polisi katika mkutano wake wa Ijumaa iliyopita chini ya uwenyekiti wa Rais Paul Kagame. Serikali ya Rwanda imekuwa ikipongezwa na nchi wafadhili kwa hatua yake ya kuwaadhibu maafisa mafisadi.  Naye Msemaji wa jeshi la polisi la Rwanda Theos Badege amesema kuwa hakuna kuonewa huruma wala kupewa msamaha maafisa polisi wanaohusika na ufisadi. Amesema ni sera ya taifa kuhakikisha kwamba vitendo vyote vya ufisadi vinakabiliwa na mkono wa sheria.
Msemaji wa Jeshi la Polisi la Rwanda, ACP Theos Badege 
Raia 200 walitiwa mbaroni mwaka jana huko Rwanda wakituhumiwa kutoa rushwa kwa polisi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages