Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, February 19, 2017

CHUI AUWA WATU SABA INDIA

Maelfu ya wanavijiji huko kaskazini mwa India wamekuwa wakiishi kwa hofu na sononeko baada ya mashambulizi ya chui kutoka katika hifadhi ya karibu na maeneo yao kudaiwa kuuwa watu saba. Gazeti la kila siku la India liitwalo "Times of India" leo hii limeandika "Chui wala watu wanatishia usalama wa vijiji 30 katika eneo la karibu na hifadhi ya chui ya Pilibhit". Wakulima ambao ndio walio wengi katika maeneo hayo ya vijijini, wanakwenda mashambani nyakati za mchana tu , wakiwa wamejihami na silaha. Watoto wanapelekwa shule kwa kusindikizwa au wanasalia nyumbani, na wanavijiji wanajiepusha kutoka nje nyakati za usiku. Afisa tawala mwandamizi Ajay Kant Saini amesema mwisho wa juma lililopita walinzi wa misitu wamefanikiwa kumkamata chui ambae anadaiwa kuwauwa wanakijiji sita tangu Novemba mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages