Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, February 6, 2017

RUSSIA: HATUKUBALIANI NA SERIKALI YA TRUMP KWAMBA IRAN NI 'DOLA LA KIGAIDI'

Russia imesema haikubaliani na mtazamo wa serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani wa kuielezea Iran kuwa ni "dola la kigaidi".
Akizungumza na kanali ya televisheni ya Fox News hapo jana, Trump alidai kuwa Iran ni "dola nambari moja la kigaidi".
Matamshi ya rais wa Marekani yanafanana na madai yaliyotolewa siku ya Jumamosi na Waziri wake wa Ulinzi James Mattis ambaye alisema Iran ni "dola mfadhili mkubwa zaidi wa ugaidi duniani".
Trump na Mattis
Akijibu matamshi hayo, msemaji wa Ikulu ya Russia, Kremlin, Dmitry Peskov amesema: "Hatukubaliani na dhana hii".
Peskov ameashiria ushirikiano na uitifaki uliopo baina na Tehran na Moscow katika masuala mbalimbali na kusisitiza kuwa Russia inakusudia kustawisha uhusiano wake na Iran.
"Nyote mnajua kwamba Russia ina uhusiano mzuri wa uitifaki na Iran, na tunashirikiana na nchi hiyo katika mambo kadhaa. Tunathamini uhusiano wetu katika uga wa biashara na uchumi na tuna matumaini ya kuustawisha zaidi uhusiano huo", amesisitiza afisa huyo wa Russia.
Dmitry Peskov
Hii ni katika hali ambayo viongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wamekanusha tuhuma za kufadhili ugaidi zinazotolewa na serikali ya Marekani na kusisitiza kwamba Tehran iko mstari wa mbele katika vita dhidi ya ugaidi.
Iran imekuwa ikitoa msaada wa ushauri wa kijeshi kwa nchi za Iraq na Syria katika vita vyao dhidi ya ugaidi. Aidha imekuwa ikishirikiana na Russia kuisaidia kijeshi serikali ya Syria katika vita hivyo…

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages