Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, April 17, 2017

WAISLAMU MAREKANI WAFANYA KONGAMANO KUBWA LA DINI TATU ZA MBINGUNI

Waislamu wa mji wa Baltimore, nchini Marekani wamefanya kongamano la 42 la kila mwaka la Waislamu wa nchi hiyo kwa kushiriki Waislamu elfu 20 kutoka maeneo mbalimbali ya taifa hilo.
Taarifa iliyotolewa na ofisi ya Kiislamu ya (ICNA) nchini Marekani imetangaza kuwa, kongamano hilo la siku tatu limejadili kadhia ya 'Juhudi kwa ajili ya Mafanikio ya kweli na Ujumbe wa Mungu wa Musa, Issa na Nabii Muhammad (saw)' hapo mjini Baltimore katika jimbo la Maryland, mashariki mwa Marekani.
Watoto wa Kiislamu katika kikao hicho
Kadhalika ofisi ya Kiislalmu ya kaskazini mwa Marekani  (ICNA) imesisitiza kuwa, katika kongamano hilo kumefanyika pia vikao mbalimbali na kujadili masuala kama vile, kukabiliana na chuki dhidi ya dini ya Kiislamu, kutetea haki za Waislamu katika kipindi cha utawala wa Rais Donald Trump, wa Marekani, ongezeko la jinai dhidi ya Waislamu na hatua hasi ya serikali ya rais huyo ya kuwazuia Waislamu kuingia nchini humo.
Obama akiwa rais alipowatembelea Waislamu wa Baltimore, Marekani
Kadhalika Waislamu nchini Marekani wamepata kutoa malalamiko yao kuhusiana na matatizo mbalimbali yanayowakabili ndani ya taifa hilo hususan baada ya kuingia madarakani Rais Trump mwenye misimamo ya kibaguzi na chuki. Wakati huo huo, zaidi ya watu 1000 wasio na makazi walipatiwa misaada mbalimbali ikiwemo ya chakula, ambayo ilitolewa na kundi la wafuasi wa dini tatu za Uyahudi, Ukristo kwa kushirikiana na Waislamu wa Baltimore.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages