Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, November 16, 2017

TAHARUKI ZIMBABWE, MUGABE ANG'ANG'ANIA MADARAKA, AU NA UN ZATOA KAULI

Taharuki Zimbabwe, Mugabe ang'ang'ania madaraka, AU na UN zatoa kauli
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ambaye yuko katika ncha ya kuuzuliwa amekataa kuachia madaraka akisisitiza kuwa yeye ndiye kiongozi halali wa nchi hiyo.
Duru za habari zimeliambia shirika la habari la Reuters kuwa, Mugabe amekataa upatanishi wa Askofu wa Kanisa Katoliki nchini humo Fidelis Mukonori, ambaye alikuwa anaongoza mazungumzo kati ya rais huyo mkongwe mwenye umri wa miaka 93 na makamanda wa jeshi la nchi hiyo.
Jeshi hilo jana lilitangaza kuwa Mugabe na familia yake wako kwenye kizuizi cha nyumbani na kuongeza kuwa litawapandisha kizimbani wale liliowataja kama "wahalifu" waliomzunguka kiongozi huyo ambao wameisababishia nchi hiyo madhara na hasara za kiuchumi na kijamii.
Makamu wa Rais wa Zimbabwe aliyefutwa kazi na kukimbilia uhamishoni
Wakati huo huo, Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kupitia msemaji wake, Farhan Haq amezitaka pande zote husika kujizuia kuchua hatua inayoweza kuvuruga mambo zaidi, na kusisitiza kuwa mgogoro uliopo unaweza kupatiwa ufumbuzi kwa njia za kisiasa na mazungumzo.
Naye Mkuu wa Umoja wa Afrika, Alpha Conde ambaye pia ni Rais wa Guinea amesema AU inalaani vikali hatua ya majenerali wa jeshi la Zimbabwe kutwaa madaraka kwa nguvu na kusisitiza kwamba mfumo wa katiba unapaswa kuheshimiwa na pande zote.
Huku hayo yakiarifiwa, Morgan Tsvangirai, kinara wa upinzani nchini Zimbabwe amerejea nchini akitokea Afrika Kusini, kufuatia kile kinachotajwa kuwa mapinduzi ya kijeshi yasiyo ya umwagikaji wa damu.
Morgan Tsvangirai
Kwa mujibu wa gazeti la NewsDay la Zimbabwe, Tsvangirai ametangaza kuwa yuko tayari kufanya mazungumzo na Emmerson Mnangagwa, Makamu wa Rais wa Zimbabwe aliyepigwa kalamu nyekundu na Mugabe hivi karibuni, kuhusu uundwaji wa serikali ya mpito.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages