Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, October 30, 2017

WATU 5 WAUAWA KATIKA MAANDAMANO DHIDI YA SERIKALI MJINI GOMA, KONGO DR

Watu 5 wauawa katika maandamano dhidi ya serikali katika mji wa Goma, Kongo DR
Maandamano ya wananchi ya kupinga serikali yaliyozusha makabiliano baina yao na polisi jana Jumatatu katika wilaya za Madjengon na Mabanga katika mji wa Goma mkoani Kivu ya Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yamesababisha vifo vya watu watano.
Maandamano hayo ambayo yalijiri jana jioni yaliitishwa na makundi ya wanaharakati wa kupigania demokrasia na mengineyo kama sehemu ya mgomo mkubwa unaoshinikiza kuondoka madarakani Rais Joseph Kabila na kudhihirisha hasira za wananchi kwa kushindwa kuendeshwa uchaguzi wa rais huko Kongo ili kumchagua rais mpya. Waandamanaji walichoma moto matairi ya gari na hivyo kusababisha msongamano wa magari katika barabara za mji wa Goma. Maandamano mengine kama hayo yanatazamiwa kufanywa siku chache zijazo.
Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo 
Mgogoro wa kisiasa Kongo DR umesababishwa na hatua ya Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo kukataa kuachia madaraka baada ya muhula wake kumalizika mwezi Disemba mwaka jana. Uchaguzi mkuu ulipangwa kufanyika nchini humo kabla ya kumalizika mwaka huu chini ya makubaliano yaliyofikiwa kati ya serikali ya Kinshasa na mrengo wa upinzani. Hata hivyo imeelezwa kuwa kushindwa kutekelezwa hatua hiyo si jambo la kushangaza kwa kuzingatia kuwa Tume ya Uchaguzi ya Kongo mwezi Julai mwaka huu ilitangaza kuwa kuna uwezekano uchaguzi huo usifanyike mwaka huu kutokana na kuwepo matatizo ya bajeti na kuendelea machafuko nchini humo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages