Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, November 29, 2017

SAFARI YA PAPA FRANCIS NCHINI MYANMAR NA MATARAJI YASIYO TEKELEZEKA

Safari ya Papa Francis nchini Myanmar na matarajio yasiyotekelezeka
Jumatatu ya tarehe 27 Novemba, Papa Francis, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani aliwasili Yangon mji mkubwa kabisa wa Myanmar akianza safari ya siku nne ya kuitembelea nchi hiyo mashariki mwa Asia.
Safari ya Papa nchini Myanmar inafanyika baada ya kupita miezi mitatu tangu kuanza duru mpya ya uangamizaji kizazi cha jamii ya waliowachache ya Waislamu Warohingya. Mamia ya Wakatoliki walijitokeza kumlaki kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki Duniani wakati alipowasili katika mji huo. Nchini Myanmar kuna Wakatoliki takribani laki saba katika jamii ya watu milioni 51 wa nchi hiyo. Wakristo hao Wakatoliki wanaishi kwa amani kamili nchini humo.
Lakini Waislamu milioni moja wa jamii ya Rohingya ambao wanapatikana katika jimbo la Rakhine la magharibi mwa Myanmar wamekuwa wakikabiliwa na ubaguzi na ukatili mkubwa pamoja na hujuma za mabudha wanaopata uungaji mkono wa serikalim katika ukatili wao dhidi ya Waislamu. Mabudha wakipata uungaji mkono wa moja kwa moja wa jeshi la Myanmar wameanzisha duru mpya ya mauaji, mateso, ubakaji wa mabinti na wanawake na kupelekea mamia ya maefu ya Waislamu hao kuwa wakimbizi.
Papa Francis, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani akiwasili Myanmar
Serikali ya Myanmar, haiwatambui Waislamu wa jamii ya Rohingya kwamba ni raia wa nchi hiyo bali inawaona kuwa ni wahajiri kutoka nchi jirani ya Bangladesh. Kabla ya kufanya safari hiyo, Askofu wa Myanmar alimtaka Papa Francis kutotumia neno Rohingya atakapokuwa safarini nchini humo, ili kuzuia kuibua hasira za viongozi wa serikali. Duru mpya ya uangamizaji kizazi cha Waislamu wa jamii ya Rohingya ilianza katika hali ambayo, jinai kama hizo hazijawahi kushuhudiwa nchini Mynamar tangu nchi hiyo ipate uhuru mwaka 1948 ambapo kabla ilikuwa ikijulikana kwa jina la Burma.
Katika kipindi cha miaka 70 iliyopita ya utawala wa Mabudha nchini humo, daima umekuwa ukitaka kukifuta kikamilifu kizazi cha jamii ya Waislamu wa Rohingya katika jimbo la Rakhine. Katika kipindi hicho Waislamu hao wameshambuliwa zaidi ya mara 20 kwa aina mbalimbali ya mashambulio. Sambamba na mashambulio hayo, kumekuweko na njama mtawalia za kuwanyima Waislamu hao haki za kiraia lengo likiwa ni kuwafuta katika ramani ya nchi hiyo. 
Papa Francis katika mazungumzo yake na Aung San Suu Kyi
Umoja wa Mataifa umetangaza katika ripoti yake kwamba, Waislamu wa Rohinga ndio jamii ya wachache ulimwenguni iliyodhulumiwa zaidi.  Tangu kuanza kwa duru mpya ya mauaji ya kizazi na utokomezaji kizazi cha jamii ya Waislamu wa Rohingya, zaidi ya Waislamu elfu moja wameuawa kikatili, makumi ya maelfu ya wanawake wamebakwa na kunajisiwa huku wengine takribani laki sita na ishirini elfu wakilazimika kuyahama makazi yao na kukimbilia katika nchi jirani ya Bangladesh. Waislamu Warohingya waliokimbilia Bangladesh nao wanakabiliwa na hali mbaya katika kambi za muda walizopatiwa kutokana na kukosa huduma muhimu za kuendeshea maisha.
Licha ya Umoja wa Mataifa na asasi za kutetea haki za binadamu kukiri bayana katika ripoti zao nyingi juu ya kutokea maafa ya kibinadamu nchini Myanmar na hali mbaya inayowakabili wakimbizi wa Kirohingya huko Bangladesh, lakini serikali ya Myanmar na hata shakhsia wake mashuhuri Aung San Suu Kyi ambaye ana Tuzo ya Amani ya Nobel wanakana kabisa juu ya kuweko muamala mbaya dhidi ya Waislamu wa nchi hiyo. 
Waislamu wa Myanmar wakiyahama makazi yao
Matamshi ya madola ya Magharibi, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani na viongozi wa Myanmar hususan Aung San Suu Kyi kuhusiana na kuhitimishwa siasa za uangamizaji kizazi dhidi ya Waislamu wa Rohingya na kuandaliwa mazingira ya kurejea wakimbizi wa jamii hiyo kutoka Bangladesh ni matarajio na utafadhalishaji. Viongozi hao badala ya kuzingatia ripoti mbalimbali za Umoja wa Mataifa na Katibu Mkuu wake kuhusiana na hali mbaya ya Waislamu Warohingya, wamekuwa wakiyapa kipaumbele matamshi ya serikali ya Myanmar.
Hivi kama badala ya Waislamu wa Rohingya, Wakristo wa nchi hiyo ndio ambao wangekuwa wanakabiliwa na siasa hizo za uangamizaji kizazi, Papa na viongozi wa madola ya Magharibi wangekuwa wanatoa matamshi kama wanayotoa hivi sasa? Je Aung San Suu Kyi angeendelea kuonekana kuwa ni fakhari kutokana na kupata Tuzo ya Amani ya Nobel? Waislamu wa jamii ya Rohingya wanauawa na wengine kulazimika kuwa wakimbizi na madola ya Magharibi yamenyamzia kimya hilo kutokana na kuwa wanaofanyiwa jinai hizo ni Waislamu na si vinginevyo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages