Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, November 19, 2017

WAFUNGWA WA KISIASA BAHRAIN WAZUILIWA KUWA NA MAWASILIANO YOYOTE NA NJE YA JELA

Wafungwa wa kisiasa Bahrain wazuiliwa kuwa na mawasiliano yoyote na nje ya jela
Duru zenye uhusiano na familia ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kitaifa ya al-Wifaq nchini Bahrain, zimeeleza kuwa utawala wa Aal-Khalifa umemwekea vizuizi vikubwa Sheikkh Ali Salman na shakhsia wengine mashuhuri wanaoshikiliwa katika jela za nchi hiyo.
Kwa mujibu wa habari hiyo, Sheikh Ali Salman na shakhsia wengine wakubwa wanaoshikiliwa katikka jela za Bahrain wamezuiliwa kufanya mawasiliano na watu wa familia zao, kupiga simu au hata kusoma magazeti. Katika kuendelea kutolewa hukumu za kidhalimu za utawala wa Aal-Khalifa dhidi ya Sheikh Ali Salman anayeendelea kutumikia kifungo cha miaka tisa jela, utawala huo umewasilisha mahakamani mashitaka mapya dhidi ya shakhsia huyo ya kile kinachotajwa kuwa eti ni kufanya ujasusi kwa maslahi ya Qatar.
Shakh Ali Salman, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kitaifa ya al-Wifaq nchini Bahrain
Katika uwanja huo, mwendesha mashtaka wa Manama amewasilisha mashtaka hayo dhidi ya Sheikh Ali Salman, Hassan Sultwan na Ali al-Usud, ambao nao pia ni wanachama wa Jumuiya ya Kitaifa ya al-Wifaq kwa tuhuma hizo hizo za kufanya ujasusi kwa ajili ya Qatar kwa lengo la kile alichokisema kuwa eti ni kutaka kuiondoa madarakani serikali ya Bahrain. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hukumu dhidi ya shakhsia hao itatolewa tarehe 27 Novemba mwaka huu.
Maandamano ya Wabahrain
Sheikh Ali Salman alikamatwa mwaka 2014 na utawala wa kidikteta wa Aal-Khalifa na kuhukumiwa kifungo cha miaka minne jela mwaka 2015 kwa tuhuma za uchochezi na kuivunjia heshima Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi hiyo. Hata hivyo mahakama ya rufaa ya nchi hiyo na katika njama za kutaka kumfunga miaka mingi zaidi shakhsia huyo ilimbadilishia mashitaka na kuyafanya ya tuhuma za kutaka kubadilisha utawala na hivyo ikamuhukumu kifungo cha miaka tisa jela.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages