Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, November 18, 2017

VELAYATI AMUONYA RAIS WA UFARANSA ASIINGILIE MAMBO YA IRAN

Velayati amuonya Rais wa Ufaransa asiingilie mambo ya Iran
Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika masuala ya kimataifa amemuonya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa asiingilie masuala ya ndani ya Iran kwani kujiingiza katika masuala yasiyomuhusu hakuna faida kwa nchi yake.
Ali Akbar Velayati amesema hayo leo wakati alipohojiwa na shirika la habari la IRIB na sambamba na kumlaumu Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kwa kuingilia masuala ya ulinzi ya Iran amesema, kitendo cha Paris cha kujiingiza katika suala la makombora ambalo ni la kiistratijia kwa Iran hakina matunda yoyote isipokuwa kuzidi kujipotezea heshima Ufaransa mbele ya Jamhuri ya Kiislamu.
Mshauri huyo wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika masuala ya kimataifa amesisitiza kuwa, Iran haiombi idhini ya mtu yeyote katika masuala yake ya kiulinzi na kusema wazi kwamba, kama Ufaransa inataka kuwa na uhusiano mzuri na Iran basi inapaswa iache kujiingiza katika masuala yake ya ndani kwani ni kinyume na maslahi ya kitaifa ya Ufaransa.
Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa

Amesisitiza kuwa, bila ya shaka yoyote majibu ya Iran kuhusu mwito wa Ufaransa juu ya mradi wake wa makombora ni hapana na hakuna hata uwezekano wa asilimia moja wa kukubaliana na jambo hilo.
Jana Ijumaa, Rais wa Ufaransa alidai eti kuna haja kwa Iran kuweka wazi stratijia zake za mradi wa makombora ya balestiki na kudai kuwa Iran inapaswa kuachana na siasa zake alizoziita eti ni za mashambulizi.
Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya kimataifa amemjibu rais huyo wa Ufaransa na kumuonya asiingilie masuala ya ndani ya Iran kwani kila nchi ina haki ya kujilinda na kwamba nchi yoyote ile haina haki ya kuipangia itumie stratijia gani katika kuimarisha nguvu zake za ulinzi. 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages