Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, November 28, 2017

UHURU KENYATTA AAPISHWA LEO NCHINI KENYA

Uhuru Kenyatta aapishwa kama rais wa Kenya
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ameapishwa kuiongoza nchi hiyo kwa muhula wa pili wa miaka mitano mjini Nairobi leo katika sherehe iliyohudhuriwa na maelfu ya wafuasi wake na viongozi kadhaa wa nchi za Afrika.
Rais Kenyatta amekula kiapo katika Uwanja wa Kasarani mjini Nairobi kufuatia ushindi wake katika uchaguzi wa marudio wa Oktoba 26 ambao ulisusiwa na kinara wa upinzani Raila Odinga kwa madai kuwa haukuwa huru na wa haki. Mahakama ya Kilele Kenya ilibatilisha uchaguzi uliokuwa umefanyika Agosti nane kwa msingi kuwa kulikuwepo na dosari.
Kati ya viongozi waliohudhuria sherehe hizo ni Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn, Marais Paul Kagame wa Rwanda, Mohamed Abdullahi Mohamed wa Somalia, Salva Kiir wa Sudan Kusini, Ian Khama wa Botswana Yoweri Museveni wa Uganda, Omar Bongo wa Gabon, Egar Lungu wa Zambia, Ismaïl Omar Guelleh wa Djibouti, na Hage Geingob wa Namibia. Tanzania imewakilishwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu baada ya Rais John Magufuli kukosa kuhudhuria kama ilivyotarajiwa. Katika hotuba yake, Rais Kenyatta ametangaza kwamba Mwafrika yeyote atapewa viza akifika katika kiingilio chochote mpakani au viwanja vya ndege Kenya.
Rais Kenyatta baada ya kuapishwa
Aidha Kenyatta amesema ana malengo mawili katika muhula wake wa mwisho. Kwanza kuimarisha uwiano na umoja miongoni mwa Wakenya. Ameongeza kuwa ameanza kuwasiliana na viongozi wote na kueleza nia yake ya kuendeleza umoja. Halikadhalika amesema lengo la pili ni kuhakikisha huduma ya afya inawafikia Wakenya 100%. Naibu wa Rais William Ruto pia ameapishwa katika sherehe hiyo.
Katika upande mwingine polisi mjini Nairobi waliliazimka kutumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya wafuasi wa Raila Odinga waliokuwa wanakutana katika uwanja wa Jacaranda katika mtaa wa Embakasi walikokuwa wamekusanyika  kuwaomboleza waliouawa katika ghasia za baada ya uchaguzi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages