Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, October 30, 2017

UHURU KENYATA ATANGAZWA RASMI MSHINDI WA UCHAGUZI WA RAIS KENYA ULIOSUSIWA NA MPINZANI WAKE

Uhuru Kenyatta atangazwa rasmi mshindi wa uchaguzi wa rais Kenya uliosusiwa na mpinzani wake
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya IEBC Wafula Chebukati amemtangaza Uhuru Kenyatta, mgombea urais kwa tiketi ya chama cha Jubilee Rais mteule na mgombea wake mwenza William Ruto kuwa Naibu Rais mteule baada ya kupata ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa marudio wa rais uliofanyika siku ya Alkhamisi.
Akitangaza matokeo hayo jioni ya leo, Chebukati alisema uchaguzi huo ulikuwa huru, halali na wa haki.
Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na mwenyekiti huyo wa IEBC, Kenyatta amejinyakulia kura 7,483,895 ambazo ni sawa na asilimia 98.27 ya kura zote halali zilizopigwa katika uchaguzi huo wa rais ambao ulisusiwa na mpinzani wake mkuu Raila Odinga.
Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati
Zoezi la kutangaza matokeo limefanyika bila kujumuisha majimbo 25 ya mkoa wa Nyanza ambayo yalishindwa kupiga kura siku ya Alkhamisi kutokana na fujo na machafuko yaliyokwamisha upigaji kura katika majimbo hayo.
Chebukati amesisitiza kuwa masharti yaliyokuwa yamewekwa na Mahakama ya Juu iliyofuta matokeo ya uchaguzi wa rais wa Agosti 8 kwa ajili ya uchaguzi wa marudio yametekelezwa, hivyo uchaguzi huo ni halali, huru na wa haki.
Aidha amesema uchaguzi wa marudio wa rais umeendeshwa na timu mpya iliyojumuisha wafanyakazi wa IEBC kutoka kila pembe ya nchi. Ameongeza kuwa hali katika majimbo 25 ya mkoa wa Nyanza ilisababisha uchaguzi ushindwe kufanyika katika maeneo hayo.
Akizungumza mapema leo, Naibu Mwenyekiti wa IEBC Consolata Nkatha alisema kura za maeneo ambayo uchaguzi haukufanyika hazitoathiri matokeo rasmi ya uchaguzi huo.
Raila Odinga
Mgombea urais kwa tiketi ya muungano wa upinzani wa NASA Raila Odinga alisusia uchaguzi wa marudio akitaka pamoja na mambo mengine kutimuliwa maafisa waandamizi wa tume ya uchaguzi na kubadilishwa wachapishaji wa karatasi za kupigia kura na watayarishaji wa teknolojia itakayotumika katika mchakato wa uchaguzi huo.
Hayo yanajiri huku Wakenya wakisubiri kwa hisia tofauti msimamo wa kiongozi huyo wa upinzani ambao ameahidi kuutangaza baada ya rais Kenyatta kutangazwa rasmi mshindi wa uchaguzi wa marudio.../

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages