Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, October 28, 2017

UHURU KENYATTA AONGOZA KWA 96%, ODINGA ATAKA UCHAGUZI MPYA NDANI YA SIKU 90

Uhuru Kenyatta aongoza kwa 96%, Odinga ataka uchaguzi mpya ndani ya siku 90
Rais Uhuru Kenyatta anaongoza kwa asilimia 96 katika matokeo ya awali ya uchaguzi wa marudio wa urais uliofanyika Alkhamisi iliyopita nchini Kenya.
Matokeo ya awali ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC) yanaonyesha kuwa Uhuru Kenyatta anaendelea kuongoza kwa kura zaidi ya milioni 7.
Wagombea wengine wanaomfuata kwa pamoja wamepata chini ya asilimia 5 ya kura zilizohesabiwa kufikia sasa.
Wananchi wa Kenya Alkhamisi walielekea kwenye masanduku ya kupigia kura katika uchaguzi wa marudio wa urais kufuatia kutenguliwa ule wa awali uliofanyika Agosti 8 mwaka huu.
Jana Ijumaa, Raila Odinga, kinara wa muungano wa NASA ambao umebadilishwa jina na sasa litafahamika kama Vuguvugu la Mageuzi NRM alisema kujitokeza idadi ndogo ya watu katika uchaguzi huo ni ishara tosha kuwa kulikuwa na uchakachuaji katika uchaguzi wa Agosti 8, huku akisisitiza kuwa lazima uchaguzi mwingine ufanyike ndani ya siku 90.
Raila Odinga
Mahakama ya Juu ya Kenya ilitengua matokeo ya uchaguzi huo wa rais kwa hoja kwamba IEBC ilifanya baadhi ya makosa katika mchakato wa uchaguzi. Muungano wa upinzani (Nasa) umewahimiza wafuasi wake kutoshiriki uchaguzi huo baada ya kiongozi wa muungano huo Raila Odinga kujiondoa katika kinyang'anyiro hicho.  
Katika hatua nyingine, IEBC imetangaza kuakhirisha tena zoezi la upigaji kura lililotazamiwa hii leo, katika kaunti nne za Kisumu, Migori, Homa Bay na Siaya, ambazo ni ngome za NASA, ambazo siku ya Alhamisi wakazi wake hawakupiga kura kwa sababu za kiusalama.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages