Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, October 28, 2017

HALI YA KIBINADAMU YEMEN INASHTUA, SAUDIA YAENDELEZA HUJUMA

Hali ya kibinadamu Yemen inashtua, Saudia yaendeleza hujuma
Mkuu wa misaada ya kibinadamu katika Umoja wa Mataifa amesema hali ya kibinadamu nchini Yemen ni ya kushtua huku Saudi Arabia ikiendeleza hujuma dhidi ya nchi hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari katika mji mkuu wa Yemen, Sana'a, Mark Lowcock ambaye Jumamosi ya leo amemaliza safari ya siku tano nchini Yemen amesema kuwa, njia pekaa ya kumaliza vita Yemen ni kupitia mchakato wa kisiasa.
Lowcock amesema hali ya kibinadamu inazidi kuzorota huku ugonjwa wa kipindupindu ukienea kwa kasi ambayo haijawahi kushuhudiwa duniani. Amesema Yemen inakabiliwa na ukosefu mkubwa zaidi wa chakula duniani na kwamba idadi kubwa ya watu wamelazimika kuwa wakimbizi.
Watoto ni waathirika wa hujuma ya Saudia nchini Yemen
Vita vamizi vya Saudia na waitifaki wake dhidi ya Yemen vilianzishwa mwezi Machi mwaka 2015 kwa kisingizio cha kutaka kumrejesha madarakani rais wa nchi hiyo aliyejiuzulu na kuitoroka nchi Abd Rabbuh Mansur Hadi. Vita hivyo vingali vinaendelea kwa mwaka wa tatu sasa bila ya utawala wa Aal Saud na waitifaki wake kufikia malengo haramu waliyokusudia. Watu zaidi ya 13,000 , wengi wakiwa ni wanawake na watoto, wameuawa katika hujuma ya Saudia nchini Yemen.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages