Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, October 21, 2017

MAREKANI YAZIDI KUJIKITA KIJESHI AFRIKA; IDADI YA ASKARI WAKE BARANI HUMO YAONGEZEKA MARA TATU

Marekani yazidi kujikita kijeshi Afrika; idadi ya askari wake barani humo yaongezeka mara tatu
Gazeti la Kifaransa la Le Monde limeripoti kuwa Marekani imepanua wigo wa uingiliaji wake kijeshi katika nchi za Afrika kwa kuongeza idadi ya askari wake walioko kwenye nchi za bara hilo.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, katika muendelezo wa sera za Washington za kudhamini maslahi yake, idadi ya askari wa Marekani wanaopelekwa katika nchi za Afrika kwa anuani ya "utoaji mafunzo, uratibu wa majeshi ya nchi za Kiafrika na kushiriki katika mapambano dhidi ya makundi ya kigaidi" imeongezeka mara tatu katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.
Ramani ya vituo vya vijeshi na vinginevyo vya Marekani barani Afrika
Le Monde limeongeza kuwa, katika harakati inayolenga kudhamini manufaa na maslahi yake barani Afrika, Marekani imekuwa ikivuruga uthabiti ndani ya nchi za bara hilo ili kuongeza idadi ya vikosi vya jeshi lake, kiasi kwamba baada ya Mashariki ya Kati, bara Afrika limekuwa eneo la pili lenye uingiliaji mkubwa zaidi wa kijeshi wa Marekani duniani.
Kwa mujibu wa viongozi wa Marekani, kati ya askari elfu nane wa kikosi maalumu cha nchi hiyo ambao tangu ulipoanza mwaka huu wa 2017 wametumwa katika pembe mbalimbali za dunia, zaidi ya askari 1,300 wako barani Afrika na wengine karibu 5,000 wako katika eneo la Mashariki ya Kati.../

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages