Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, October 28, 2017

WAFUNGWA ZAIDI YA ELFU MOJA WA JELA YA TORA MISRI WAANZA MGOMO WA KULA

Wafungwa zaidi ya elfu moja wa jela ya Tora Misri waanza mgomo wa kula
Wafungwa wa jela yenye ulinzi mkali ya Tora mjini Cairo Misri wameanza mgomo wa kula chakula wakipinga mazingira mabaya yanatotawala jela hiyo.
Zaidi ya wafungwa elfu moja wa jela hiyo maarufu kwa jina la Jela la Nge wamenza mgomo wa kula wakilalamikia kunyimwa haki zao za kimsingi ikiwa ni pamoja na kuzuiwa jamaa zao kuwatembelea, kunyimwa huduma za afya na kadhalika.
Wakili Usama Biyumi anayeshughulikia kesi za wafungwa kadhaa wa jela hiyo amesema kuwa, ukatili wa idara ya jela hiyo dhidi ya wafungwa unaongezeka siku baada ya siku licha ya matakwa ya kukomeshwa mienendo hiyo.
Anesema kuwa maafisa wa jela hiyo wamekuwa wakizuia kuingizwa chakula kwa wafungwa na kupewa vyakula visivyokuwa salama.
Familia za wafungwa mbele ya jela ya Tora, Cairo
Biyumi ameongeza kuwa, mgomo huo ulianzishwa siku kadhaa zilizopita na baadhi ya wafungwa, na wafungwa wengine wa jela hiyo wamejiunga na wenzao hao baada ya matakwa yao kukataliwa na idara ya jela hiyo.
Wafungwa wa jela hiyo wananyimwa haki za kimsingi na manyanyaso yanashadidi zaidi kwa wafungwa wa kisiasa ambao wanashikiliwa katika seli zenye giza totoro na wanazuiwa kuzungumza na wenzao.
Misri imekuwa ikikosolewa na mashirika ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu kutoka na ukatili na manyanyaso yanayofanywa dhidi ya wafungwa katika jela za nchi hiyo. 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages