Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, June 13, 2017

WATU 15 BAADA YA JENGO KUPOROMOKA

Watu 15 hadi sasa hawajulikano waliko baada ya jengo la ghorofa saba kuporomoka katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi Jumatatu usiku.
Kamanda wa Polisi Nairobi Japheth Koome anasema watu 121 waliokolewa punde baada ya jingo hilo kuporomoka saa nne usiku katika mtaa wa Kware eneo la Embakasi mashariki mwa Nairobi.
Koome amesema kuna wakaazi takribani 15 wa jengo hilo ambao hawajulikano waliko kwani baadhi walikataa kuondoka wakati walipotakiwa kufanya hivyo jengo lilipoonekana linaelekea kuporomoka.
Msemaji wa Idara ya Kitaifa ya Kukabiliana na Maafa  Pius Masai amesema familia nyingi zilishirikiana na kuweza kuondolewa katika jengo hilo lakini bado waokoaji wanajaribu kuwatafuta watu wanaoaminika kufunikwa na vifusi.
  • Gavana wa Nairbi Evans Kidero alitembelea eneo la tukio na kusema jengo hilo limejengwa kinyume cha sharia. Aidha amesema majengo 30,000 Nairobi yanatakiwa kubomolewa kwa sababu yamejengwa kwa viwango duni na ni hatari kwa maisha ya wakazi. Mwaka jana watu 50 walipoteza maisha wakati jengo lilipoporomoka katika mtaa wa Huruma mjini Nairobi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages