Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, June 12, 2017

11 WAUAWA HUKU WAFUNGWA WAPATAO ELFU MOJA WAKITOROKA JELA KONGO DR

Watu wasiopungua 11 wameuawa huku wafungwa 930 wakitoroka jela wakati watu wenye silaha wasiojulikana walipovamia jela moja iliyoko kwenye mji wa Beni, kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Gavana wa mkoa wa Kivu Kaskazini Julien Paluku ametangaza kupitia taarifa kuwa katika uvamizi huo uliotokea jana, washambuliaji hao walitumia silaha nzito nzito na kuwaua walinzi wanane wa jela hiyo.
Shambulio hilo la jana ni la nne kwa akali la utorokaji jela kutokea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ndani ya kipindi cha mwezi mmoja uliopita, likionyesha ni jinsi gani hali ya ukosefu wa usalama ilivyoongezeka nchini humo tangu Rais Joseph Kabila alipokataa kungátuka madarakani baada ya muhula wake wa uongozi kumalizika mwezi Desemba mwaka jana.

Rais Joseph Kabila 

Teddy Kataliko, ambaye ni mwanaharakati katika mkoa wa Kivu Kaskazini amesema haijaweza kufahamika ni nani hasa waliofanya shambulio hilo la kuvamia jela kwa sababu wanamgambo wengi wanaojihami kwa silaha ambao wanajulikana kama Mai Mai wanaendesha harakati zao katika mji wa Beni.
Kwa mujibu wa Polisi, wafungwa wapatao 4,000 walitoroka jela mwezi uliopita katika jela yenye ulinzi na usalama wa hali juu iliyoko kwenye mji mkuu wa Kongo DR, Kinshasa ambapo kundi la watu wanaopigania kujitenga lilihusishwa na hujuma hiyo. Wafungwa wengine wasiopungua watatu walitoroka katika jela nyengine ya mjini Kinshasa siku ya Jumamosi iliyopita.../

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages