Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, December 30, 2016

SERIKALI YA MISRI YAPITISHA MPANGO WA KUIPATIA SAUDIA VISIWA

Ripoti kutoka Misri zinaeleza kuwa licha ya malalamiko ya wananchi na upinzani wa mahakama, serikali ya nchi hiyo imepitisha mpango wa kuipatia Saudi Arabia visiwa viwili vya Tiran na Sanafir. Duru za habari za Misri zimetangaza kuwa serikali imeidhinisha mpango huo na tayari imeshaupeleka bungeni.
Kwa mujibu wa duru hizo, Mahakama Kuu ya Misri imepinga mpango huo na inatazamiwa kutoa hukumu yake rasmi juu ya suala hilo katika kipindi cha wiki mbili zijazo.
Baadhi ya shakhsia na wataalamu wa sharia nchini Misri wanaitakidi kuwa uamuzi wa kupitishwa mpango wa kuipatia Saudia visiwa viwili ambavyo Wamisri waliowengi wanaamini ni milki ya nchi yao una uhusiano na kadhia ya kamati za sharia za bunge la Misri.
Ahmad Suleiman, waziri wa zamani wa sharia ameashiria suala hilo na kueleza kwamba lengo la mpango huo ni kukabiliana na mahakimu wanaotoa hukumu kinyume na matakwa ya viongozi wa serikali na badala yake kuzingatia maslahi ya taifa tu. Ameongeza kuwa lengo la serikali ni kuwaondoa mahakimu wanaotoa hukumu zisizoendana na mitazamo ya serikali.
Rais Abdel Fattah el Sisi wa Misri (kulia) na Mfalme Salman wa Saudi Arabia
Mapema mwaka huu, serikali ya Misri ilitiliana saini mkataba wa mipaka ya bahari na Saudia na kutangaza kufuatia hatua hiyo kwamba visiwa vya Tiran na Sanafir viko kwenye maji ya ardhi ya Saudia.
Imeelezwa kuwa serikali ya Cairo itapatiwa dola bilioni 20 na Saudi Arabia kwa kuupatia utawala wa kifalme wa Aal Saud visiwa hivyo.
Uamuzi huo umelaaniwa na kulalamikiwa vikali na wananchi, duru za kisiasa, vyombo vya habari na asasi za kiraia nchini Misri ambao wamemtuhumu Rais Abdel Fattah el Sisi kuwa amefanya uhaini na kuziuza ardhi za nchi hiyo.
Hata hivyo katika jibu alilotoa kuhusiana na tuhuma hizo El Sisi amesema hajaipatia Saudia hata chembe ya ardhi ya Misri bali ameirejeshea nchi hiyo haki yake…/

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages