Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, December 30, 2016

MAMIA YA MATAKFIRI WANAOREJEA TUNISIA WAKAMATWA

Msemaji wa serikali ya Tunisia ametangaza habari ya kukamatwa mamia ya matakfiri wanaorejea nchini humo kutoka eneo la Mashariki ya Kati.
Iyad Dahmani, msemaji wa serikali hiyo amesema kuwa tokea mwaka 2007 hadi sasa matakfiri wapatao 800 wa Kitunisia wametiwa mbaroni na kufungwa jela baada ya kurejea nchini humo kutokea Syria, Iraq na Libya na kwamba hivi sasa wako chini ya uangalizi mkali. Akizungumzia suala hilo hivi karibuni, Youssef Chahed, Waziri Mkuu wa Tunisia amesema kuwa serikali yake haijatia saini mkataba wowote wa kurejeshwa nchini humo magaidi wa kitakfiri na kwamba  serikali hiyo haiungi mkono kurejea nchini humo kwa magaidi hao.
Youssef Chahed, Waziri Mkuu wa Tunisia
Wiki iliyopita, Hadi Majdub, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tunisia alitangaza habari ya kurejkea nchini matakfiri 800 na kuongeza kuwa viongozi wa nchi hiyo wana habari kamili kuhusiana na magaidi hao. Tokea kuanza kwa vita huko Syria maelfu ya Watunisia waliamua kujiunga na kundi la kigaidi la Daesh na kushiriki katika vitendo vya kinyama na kigaidi dhidi ya wananchi wa Syria. Hata hivyo katika miezi ya hivi karibuni ambapo kundi hilo limekuwa likidhoofika siku baada ya siku kufuatia kushindwa katika medani za vita katika nchi hiyo na Iraq, wanachama wa Daesh wamekuwa wakitafuta njia za kurudi katika nchi zao, jambo ambalo limewatia wasiwasi mkubwa viongozi wa nchi hizo na hasa wa Tunisia.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages