Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, December 30, 2016

NDEGE YA UTURUKI YAWAHAMISHIA YEMEN MAGAIDI WA ISIS KUTOKA ALEPPO

Duru za Yemen zimeripoti kuwa, ndege moja ya Uturuki imewahamishia nchini humo makumi ya magaidi wa Daesh (ISIS) kwa kutumia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Aden, kusini mwa Yemen, baada ya magaidi hao kufurushwa nchini Syria.

Mtandao wa habari wa al Masirah wa Yemen umeripoti kuwa, ndege ya Uturuki iliyokuwa na magaidi 150 waliofurushwa katika mji wa Halab (Aleppo) wa kaskazini magharibi mwa Syria, imetua katika uwanja huo, ikiwa ni uingiliaji wa wazi wa masuala ya ndani ya Yemen. Tarehe 22 Disemba mwaka huu, jeshi la Syria lilitangaza kukombolewa kikamilifu mji wa Halab baada ya magaidi wote kuukimbia mji huo baada ya kuukalia kwa zaidi ya miaka minne.

Duru za usalama za Yemen zimetangaza kuwa, ndege ya Uturuki iliyowabeba magaidi hao iliongozwa na vikosi vamizi ya Umoja wa Falme za Kiarabu ambavyo vinashiriki katika mashambulizi ya kivamizi yanayoongozwa na Saudi Arabia dhidi ya wananchi wa Yemen.


Vile vile mtandao wa habari wa al Masirah umesema kuwa, ndege hiyo ya Uturuki itabeba mamluki 158 wa Saudi Arabia waliojeruhiwa na wanajeshi na vikosi vya wananchi wa Yemen katika mkoa wa Ta'izz. Majeruhi hao watatibiwa katika hospitali za Uturuki. Uturuki inatajwa kuwa moja ya waungaji mkono wakuu wa magenge ya kigaidi nchini Syria kama ambavyo pia inalaumiwa kwa kutoa mafunzo kwa magenge ya kigaidi yanayofanya jinai ndani ya Syria.
Hadi sasa mashambulizi ya kivamizi yanayoongozwa na Saudi Arabia huko Yemen yameshaua watu zaidi ya 11,400, kwa mujibu wa kundi la haki za binadamu lisilo la kiserikali la Yemen lijulikanalo kwa jina la Kituo cha Kisheria kwa Ajili ya Haki za Binadamu na Maendeleo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages