Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, December 4, 2017

RAIS WA ZAMANI WA YEMEN, ALI ABDULLAH SALEH, AUAWA, WIZARA YATOA TAMKO

Rais wa zamani wa Yemen, Ali Abdullah Saleh, auawa, wizara yatoa tamko

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Yemen imetoa tamko na kuthibitisha habari ya kuuawa rais wa zamani wa nchi hiyo, Ali Abdullah Saleh.

Leo jioni Wizara ya Mambo ya Ndani ya Yemen imesema katika tamko lake kwamba Ali Abdullah Saleh, ameuawa.

Yahya al Mahdi, mkuu wa idara ya itikadi katika jeshi la Yemen naye amethibitisha habari ya kuuawa Ali Abdullah Sale na kusema kuwa, rais huyo wa Yemen ameuawa wakati alipokuwa akikimbia kutoka mjini San'a kuelekea Ma'rib.


Rais wa zamani wa Yemen, Ali Abdullah Saleh

Amesema, vikosi vya usalama vya Yemen leo Jumatatu viligundua njia aliyokuwa anatumia Ali Abdullah Saleh kutoka eneo moja kwenda eneo jingine na walipata taarifa za kiitelijinsia za namna wafuasi wake walivyokuwa wanapanga kumtorosha San'a na kumkimbiza mafichoni Ma'rib.

Mkuu huyo wa idara ya itikadi ya jeshi la Yemen ameongeza kuwa, maafisa usalama wa nchi hiyo walianza operesheni ya kumtia mbaroni Ali Abdullah Saleh mara alipofika katika eneo la Sanhan. Hata hivyo walinzi wake hawakuwaruhusu maafisa usalama wa Yemen kumtia mbaroni na hapo ukatokea ufyatulianaji risasi baina ya pande mbili ambao umeishia kwenye kuuawa Ali Abdullah Saleh na viongozi wengine wa ngazi za juu wa chama chake. 

Habari ya kuuawa Ali Abdullah Saleh imethibitishwa pia na picha kadhaa pamoja na mkanda wa video ulioenea katika mitandao ya kijamii.


Viongozi wa zamani wa Tunisia, Yemen, Libya na Misri waliopinduliwa katika miaka ya hivi karibuni



Kuanzia siku chache zilizopita, mji mkuu wa Yemen, San'a umekuwa ukishuhudia mapigano baina ya makundi yenye silaha ya Ali Abdullah Saleh na jeshi na kamati za kujitolea za wananchi zenye mfungamano na harakati ya Answarullah.

Taarifa zinasema kuwa, fitna ya hivi sasa iliyoanzishwa na rais wa zamani wa Yemen dhidi ya harakati ya Answarullah na uhusiano wa karibu wa Ali Abdullah Saleh na Saudi Arabia ni katika njama zilizokuwa zinaendeshwa na Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) za kutaka kuurudisha madarakani ukoo wa Ali Abdullah Saleh nchini Yemen.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages