Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, December 4, 2017

JESHI LA POLIS LA TANZANI NA RWANDA YAUNGANA KWA AJILI YA KUPAMBANA NA UHALIFU


Majeshi ya Polisi ya  Tanzania na Rwanda yaungana kwa ajili ya kupambana na uhalifu
Tanzania na Rwanda zimeunganisha nguvu kupitia majeshi yao ya polisi chini ya wakuu wake IGP Simon Sirro wa Tanzania na Emmanuel Gasana wa Rwanda ili kupambana na uhalifu, ujangili na kuangalia namna ya kutatua matatizo ambayo yanazikumba nchi hizo.
Akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam  Emmanuel Gasana, Mkuu wa Jeshi la Polisi la Rwanda amesema kuwa, lengo ni pande mbili kushirikiana kutokana na changamoto ambazo zinatokea katika nchi mbili hizo likiwemo suala la kuongeza nguvu, teknolojia, vifaa na kuongeza uzoefu wa matumizi ya vifaa.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania IGP Simon Sirro
Kwa upande wake, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania IGP Simon Sirro amesema kuwa, ushirikiano huo  unafanyika kwa kuangalia nini ambacho kinatakiwa kufanywa na maarifa ambayo yatatumiwa ili Jeshi la Polisi liweze kufanya kazi yake kwa usahihi na kupunguza uhalifu na endepo mtu akijiingiza kwenye uhalifu anaweza kupoteza familia yake na kuishia pabaya.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania IGP Simon Sirro amesema kuwa, “Wenzetu Rwanda wako mbele katika matumizi ya teknolojia, hivyo kuna baadhi ya mambo ambayo watatuelekeza na tutapata uzoefu katika kupambana na wahalifu wa mitandaoni ambao wamekuwa wakiwasumbua raia katika nchi yetu.
Emmanuel Gasana, Mkuu wa Jeshi la Polisi la Rwanda

Aidha IGP Simon Sirro ameongeza kuwa, sisi pia tuna uzoefu wa mambo mengi ambayo wenzetu Rwanda watajifunza kutoka kwetu na hivyo tunaweza kusema kuwa, kila mmoja katika ushirikiano huo anaweza kumpatia mwenzake uzoefu alionao hasa katika suala zima la kupambana na uhalifu

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages