Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, May 21, 2018

KIMBUNGA CHA KITROPIKI CHAIKUMBA SOMALILAND; WATU WASIOPUNGUA 15B WAAGA DUNIA

Watu wasiopungua 15 wameaga dunia huko Somaliland baada ya mvua kubwa zilizosababishwa na kimbunga cha kitropiki kwa jina la Sagar kuiathiri nchi hiyo ya Pembe ya Afrika mwishoni mwa wiki.
Somaliland ilijitenga  na Somalia mwaka 1991. Abdirahman Ahmed Ali Gavana wa eneo la Awdal amesema kuwa mvua kubwa zilizonyesha katika muda wa masaa 24 yaliyopita zimeua watu 16 katika wilaya za Lughaya na Baki. Serikali ya Somaliland tayari imeanza kutoa misaada ya dharura kwa wahanga wa kimbunga hicho. Wakati huo huo upepo mkali uliosababishwa na kimbunga cha Sagar umewasomba wanaume wawili pamoja na gari yao huko katika mji wa Bosaso katika eneo la Puntland, huko kaskazini mashariki mwa Somalia. Hayo yameelezwa na Yusuf Mohamed Waeys Gavana wa Bari katika eneo la Puntland.
Wakati huo huo Ofisi ya Umoja wa Mataifa Inayohusika na Uratibu wa Masuala ya Kibinadamu imesema kuwa maelfu ya watu wameathirika na mafuriko hayo, wamepoteza makazi na miundo mbinu kuharibiwa huko Puntland.   
Kimbunga cha kitropiki cha Sagar kilivyoiathiri Somaliland 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages