Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, September 12, 2017

MASHIRIKA YA KUTETEA HAKI ZA BINADAMU YAIKOSOA UN KWA KUTOCHUKUA HATUA DHIDI YA MAUAJI YA WAISLAMU, MYANMAR

Jumuiya na mashirika ya kutetea haki za binadamu yamelikosoa vikali Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutokana na kutochukua msimamo imara mbele ya jinai zinazoendelea kufanywa na jeshi na Mabudha wa Myanmar dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini humo.
Mashirika hayo yanasema kinachofanyika nchini Myanmar ni maangamizi ya kizazi cha Waislamu wa Rohingya.
Mashirika hayo yameashiria jinai ya kuwalazimisha Waislamu zaidi ya laki tatu wa Myanmar kuyahama makazi yao katika kipindi cha kuanzia tarehe 25 mwezi uliopita na kusisitiza udharura wa kusitishwa uhalifu kama huo. Mashirika hayo pia yamezitaka nchi wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zinazotazamiwa kukutana leo mjini New York kwa ajili ya kuchunguza mgogoro wa Myanmar, zichukua hatua za maana katika uwanja huo. 
Waislamu wa Myanmar wakilazimishwa kuhama makazi na vijiji vyao
Siku chache zilizopita pia Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran, Muhammad Javad Zarif alimwandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua za kusitisha ukatili unaofanyika kwa mpangilio maalumu dhidi ya Waislamu nchini Myanmar.
Tangu Ijumaa ya tarehe 25 Agosti Waislamu wasiopungua elfu 6 na 334 wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar wameuwa na wengine zaidi ya elfu 8 kujeruhiwa katika wimbi jipya la mashambulizi na ukandamizaji unaofanywa na jeshi la nchi hiyo dhidi ya Waislamu katika mkoa wa Rakhine.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages